FURSA UZALISHAJI WA MIWA

Kutokana na ongezeko la watu na ukuaji wa kipato miongoni mwa watanzania, ukuaji wa soko la sukari Tanzania unakadiriwa kufikia asilimia 6% kwa mwaka. Upungufu wa usambazaji wa sukari kwa sasa unakadiriwa kufika tani 300,000.
Takwimu hizi zinategemewa kupanda kwa kasi kwa sababu wazalishaji wa sukari waliopo hawajaongeza uwezo wao wa kuzalisha kulingana na ukuaji wa mahitaji. Mbali na upungufu huo ndani ya Tanzania, upungufu wa sukari kwa soko la Afrika Mashariki unakadiriwa kufikia tani 400,000 kwa mwaka. Kwa kuzingatia hayo uzalishaji wa sukari ni fursa ambayo wajasiriamali kwa ujumla wanatakiwa kuitumia ili kujiongezea kipato. Mikoa kama Kagera na Morogoro ndio mikoa ambayo kilimo cha miwa kinashamiri vizuri.